Tuesday, May 31, 2016

CHANZO CHA MATESO YA BENARD MWINJE IKO TAYARI... SOMA HAPA...


Benard Peter Mwinje
Mwimbaji wa nyimbo za injili na Mwalimu wa Kwaya Benard Peter Mwinje ameliambia Jicho Wazi kuwa tayari amekamilisha kupika Album yake yenye jumla ya nyibi Nane( 8)
Album hiyo iliyobeba jina la CHANZO CHA MATEZO, itaanza kupatikana mitaani hivi karibuni kwani kila kitu kiko tayari.
"... kusema kweli namshukuru Mungu kwani nimemaliza Kuandaa album yangu ambayo ina kwenda kwa jina la Chanzo cha mateso, wengi walidhani ntafeli lakini kwauwezo wa Mungu nimemaliza na hivi karibuni ntaaza kuisambaza kwani kama unavyoona hii hapa ndio kava lake ambalo nimetengeneza na Kampuni ya MO Design..." Alisema Mwinje.
akaongeza kuwa ataanza kuuza Audio tu peke yake ili apate pesa ya kuongezea katika maandalizi aliyonayo ya kufanya Video. Mwinje pia aliweka wazi kuwa yuko tayari kupokea mialiko mbalimbali kwani anachokifanya ni huduma ambayo iko ndani yake na kazi ambayo ametumwa na Mungu wake.
Nyimbo ambazo zinpo katika Album hii ya Chanzo Cha Mateso ni pamoja na. Chanza cha Mateso, Ukiwa na Raha, Mbinguni, Dhahabu, Duniani, Kwa neema, Nijifiche wapi pamoja na Mungu Wangu.

CHANGAMOTO: NI COVER IPI KATI YA HIZI INAFAA KUTUMIWA NA MWIMBAJI AGNESS NKUNGWE?.. USHAURI WAKO...


Mwimbaji Agness Nkungwe
Hakuna kazi duniani inayokosa changamoto, unaweza ukafanya kitu katika maisha wewe ukaona uko sahihi lakini jicho la pembeni likaona unachapia,
Hata katika kazi hizi za kudesign Cover na posters, watu wanakutana na changamoto nyingi zingine ukiziangalia zinakuwa hazina msingi lakini ilimradi tu nichangamoto imetoke.
katika kulichunguza hili, Jicho Wazi tulitazama hizi Cd Cover zilizotengenezwa na MO Design na tukaambiwa kuwa moja kati ya hizi ndio ilikuwa sahihi lakini mwenyewe alivyozitazama akaikataa na kisha kuomba mabdadiliko.


Sasa Jicho Wazi tungependa kuwaomba watazamaji na ninyi mjaribu kuzitazama hizi Cd Cover za Mutumishi na Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Agness Nkungwe kisha mtuambie ni ipi kati ya hizi mbili ambayo inafaa kutumiwa na huyu mtumishi. Agness Nkungwe.
Isiwe changamoto zingine zinaletwa tu na ushauri wa watu wengi na kukufanya wewe mwenyewe ushindwe kafanya maamuzi.

Thursday, May 26, 2016

HUDUMA YA MAACHILIO... UKOMBOZI NI HAKI YAKO... JUMAPI HII...



Jumapili hii Katika Viwanja vya Sifa zamani kama Viwanja vya Fisi, kutakuwa na HUDUMA YA MAACHILIO Itakayojulikana kama UKOMBOZI NI HAKI YAKO.... ibada hizi zitakuwa chini ya Apostle Paul Kaisi na Nabii Debora Kaisi... Hivyo unaombwa kufika bila kukosa ili ukutane na Mwisho, Huzuni, vilio visivyoisha katika ndoa yako, Kazi zako, Biashara zako na Mwengine Mengi.

Huduma Hii itakuwa kama ifuatavyo, IBADA YA KWANZA ITAANZA SAA1:00 Mpaka SAA 3:00 ASUBUHI... Wakati IBADA YA PILI ITAANZA SAA4:00 Mpaka SAA 7:30 MCHANA.

Njoo ukutane na Watumishi wa Mungu ili Ukombozi wako utimie... KUMILIKI NA KUTAWALA NI HAKI YAKO.

Wednesday, May 25, 2016

ALFREDY FUNDA NA UMELIBEBA KUSUDI... HII NI MPYA KABISA...


Mwimbaji wa nyimbo za Injili lfred Funda

Huduma na Machozi Futa Machozi LIBEBE KUSUDI lako ukilibeba kusudi lazima wachawi wakutege komaa mwanangu mlilie Mungu maana anakusudi LA kukuleta duniani usishindane na mpumbavu atakuvunjia kusudi lako .....komaa

Haya ni maneno aliyoyaandika leo katika ukurasa wake wa Facebook Mwimbaji huyu wa nyimbo za injili Alfred Funda na ambaye anatamba kwa sasa na kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la UMELIBEBA KUSUDI, kibao kilichotengenezwa katika Studio za Sandtone Records chini ya Producer Benja. wimbo huu ni katika mtiririko wa nyimbo zake nyingi ambazo tayari ameshaziandaa kwa ajili ya album yake.

Alfred Funda anaendelea kufanya vizuri katika wito wake na katika kulibeba Kusudi lake, ukilinganisha na huko aliko tokea ambapoa alikuwa anamwimbia Mungu kweli lakini katika mtindo wa Hip hop Gospel, hakuna aliyefikiria kuwa Funda ana sauti nzuri katika kuimba, na kama huamini basi utafute wimbo wake mpya huu ambao unatamba maredioni utaamini nikisemacho, kama hujaupata basi piga simu katika vituo vya redio wataucheza utajihakikishia niksemacho.