
Mwimbaji wa nyimbo za Injili lfred Funda
Huduma na Machozi Futa Machozi LIBEBE KUSUDI lako ukilibeba kusudi lazima wachawi wakutege komaa mwanangu mlilie Mungu maana anakusudi LA kukuleta duniani usishindane na mpumbavu atakuvunjia kusudi lako .....komaa
Haya ni maneno aliyoyaandika leo katika ukurasa wake wa Facebook Mwimbaji huyu wa nyimbo za injili Alfred Funda na ambaye anatamba kwa sasa na kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la UMELIBEBA KUSUDI, kibao kilichotengenezwa katika Studio za Sandtone Records chini ya Producer Benja. wimbo huu ni katika mtiririko wa nyimbo zake nyingi ambazo tayari ameshaziandaa kwa ajili ya album yake.
Alfred Funda anaendelea kufanya vizuri katika wito wake na katika kulibeba Kusudi lake, ukilinganisha na huko aliko tokea ambapoa alikuwa anamwimbia Mungu kweli lakini katika mtindo wa Hip hop Gospel, hakuna aliyefikiria kuwa Funda ana sauti nzuri katika kuimba, na kama huamini basi utafute wimbo wake mpya huu ambao unatamba maredioni utaamini nikisemacho, kama hujaupata basi piga simu katika vituo vya redio wataucheza utajihakikishia niksemacho.
No comments:
Post a Comment