Saturday, July 9, 2016

BEATRICE KITAULI WA MAUA ANG'ATWA NA NYOKA AKIWA LOCATION...




Hakuna kazi Duniani ambayo Binadamu yeyote anaweza kuifanya ikakosa changamoto, lakini pia unaambiwa ukiona changamoto zimekuwa nyingi ujue mafanikio yanakaribia.
Muimbaji wa nyimbo za injili na ambaye anatamba na kibao cha MAUA, Beatrice Kitauli, aling'atwa na nyoka akiwa katika ukaguzi wa Location kwa ajili ya shooting ya wimbo wa MAUA.
Akiongea na mtandoa pacha wa mtandao huu, (JICHO WAZI), Beatrice amesema kuwa nyoka huyo aliibuka ghafla na kumng'ata mguuni, lakini aliwahi kupatiwa huduma za haraka zilizozuia sumu kusambaa na sasa anaendelea vizuri.

Beatice amewaomba Mashabiki wake wasiwe na hofu kwani anaendelea vizuri na kazi ya kuhakikisha Video ya Album ya MAUA inakamilika kwa msaada wa Mungu, lakini pia ameomba msaada wa maombi kwani bila maombi hawezi kufanikisha.
Mitandao ya MO Designtz, Jicho Wazi na Soka Sport Inakupa pole sana Beatrice na Mungu awe nawe ili ukamilishe Kazi zako salama.

No comments:

Post a Comment