Wednesday, July 13, 2016

IKO HAPA SABABU YA ASKOFU GWAJIMA KUKAMATWA NA POLISI UWANJA WA NDEGE DAR...


Gwajima
Askofu wa kanisa la ufufuo na uzima Josephat Gwajima jana July 12 2016 amekamatwa na polisi wakati anawasili Tanzania kutokea ughaibuni ambapo baada ya kukamatwa alichukuliwa na kuhojiwa kwa saa kadhaa kituoni.
Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro amesema Gwajima amehojiwa kutokana na kauli yake ya uchochezi aliyoitoa kabla hajasafiri kwenda nje ya nchi. kamanda sirro amesema kuwa tayari walishamuhoji na upelelezi unaendelea.
Alipofika tu uwanja wa ndege alichukuliwa, yeye alifikiri anaweza tu kuja kimyakimya bila kuonekana…. uwezekano wa kutoonekana ni mdogo sana, tumeshamuhoji vizuri upelelezi unaendelea na tukipata ushahidi wa kutosha sheria itachukua mkondo wake, yuko nje kwa dhamana‘ – alisema Sirro.

Saturday, July 9, 2016

BEATRICE KITAULI WA MAUA ANG'ATWA NA NYOKA AKIWA LOCATION...




Hakuna kazi Duniani ambayo Binadamu yeyote anaweza kuifanya ikakosa changamoto, lakini pia unaambiwa ukiona changamoto zimekuwa nyingi ujue mafanikio yanakaribia.
Muimbaji wa nyimbo za injili na ambaye anatamba na kibao cha MAUA, Beatrice Kitauli, aling'atwa na nyoka akiwa katika ukaguzi wa Location kwa ajili ya shooting ya wimbo wa MAUA.
Akiongea na mtandoa pacha wa mtandao huu, (JICHO WAZI), Beatrice amesema kuwa nyoka huyo aliibuka ghafla na kumng'ata mguuni, lakini aliwahi kupatiwa huduma za haraka zilizozuia sumu kusambaa na sasa anaendelea vizuri.

Beatice amewaomba Mashabiki wake wasiwe na hofu kwani anaendelea vizuri na kazi ya kuhakikisha Video ya Album ya MAUA inakamilika kwa msaada wa Mungu, lakini pia ameomba msaada wa maombi kwani bila maombi hawezi kufanikisha.
Mitandao ya MO Designtz, Jicho Wazi na Soka Sport Inakupa pole sana Beatrice na Mungu awe nawe ili ukamilishe Kazi zako salama.