Monday, July 31, 2017

ISAYA MSANGI AWASHA MOTO MKALI SANA MWANZA... TAZAMA HAPA...



Mwimbaji wa Nyimbo za injili Nchini Tanzania Isaya Msangi, amefanya kufuru katika ibada za Jumapili alizokaribishwa kuhudumu huko Jijini Mwanza katika kanisa la Ukombozi na kuwafanya waumini kupagawa kwa nyimbo zake mbili mpya alizoimba.

Akizungumza na Gospel 1 Magazine Isaya Msangi Ambaye pia ni daktari wa maginjwa ya binaadamu, amesema kuwa hakutegemea mapokeo ya kiasi hicho kwani nyimbo hizo ni mpya na hazina promo bado, lakini ameshangazwa na jinsi watu walivyozipokea nyimbo hizo kwani watu hawakutaka hata kukaa chini.

"... hakika nimeuona mkono wa Mungu katika ujio wa Nyimbo zangu hizi imbili ambazo nilikuwa bado sijazitambulisha rasmi, lakini kwa moto ulivyowaka pale Mwanza kusema ukweli, mkono wa Mungu uko juu yangu... naamini kabisa nyimbo hizi zitakuja kuwa kuja moto wa kuotea mbali..."

Isaya amewasha moto huo katika kanisa la Ukombozi chini ya Mchungaji BG Malisa Jijini Mwanza - Tanzania ambapo aliimba nyimbo zake mpya Kimeeleweka na Leo ni Zamu Yako.

TAZAMA VIDEO HAPA

Wednesday, July 26, 2017

EBENEZA WIMBO WA MWAKA... NI CHANGAMOTO KWA WAIMBAJI WA INJILI...



Muimbaji wa wa Kitambo na Producer wa Kitambo na Kijana mwenye vipaiji vingi, wenyewe wanasema Muhenga, Mussa Sikabwe, ametangaza kuachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la EBENEZA, Ukiwa ni wimbo uliotengenezwa na kuimbwa katika viwango vingine.

Akizungumza na Gospel 1 MagazineMussa Sikabwe maarufu kwa Jina la MO, amesema kuwa ameamua kuachia wimbo huo ikiwa kama ni utambulisho wake rasmi katika Tasnia ya nyimbo za Injili, kwani hapo nyuma ni kweli alikuwa anaimba Gospel lakini alikuwa bado hajaingia kabisa.

"... unajua kila kitu ni wito, na hii kazi yaMungu tunafanya kulingana na Wito... kila mtu kanisani ameitwa kwa Karama yake, kun walioitwa kwa Uchungaji wapo walioitwa kwa ushemasi, Uinjilisti na vipawa vingine vingi, lakini mimi ni meitwa kwa Uimbaji, lakini bado muda wangu ulikuwa haujafika... alisema Mussa.

"... sio kuwa nilikuwa siimbi kabisa hapana, hata ukiingia you tube utakuta nyimbo yangu nyingine, lakini nasema tu muda wangu ulikuwa haujatimia, lakini kwa sasa ninaamini kuwa Mungu sasa ameniruhusu nianze Rasmi na ndio maana nimeamua nianze na Wimbo huu uitwao EBENEZA. ameendelea kusema Mussa

Mussa amesema kuwa pamoja na Ebeneza kwa sasa ana nyimbo nyingine tatu, ambapo mmpja alishauweka you tube tayari unaitwa DAMU SUKUMA MOYO, lakini pia yuko mbioni kukamilisha nyimbo zilizobaki zitakazo kuwa ndani ya Album ya Ebeneza.

amesema kuwa hivi karibuni atatoa kwanza video ya wimbo huu wa Ebeneza wakati akiwa anaendelea kumalizia audio zilizobaki katika albabu yake.

Mussa Sikabwe amesema kuwa yeye yuko tayari kwa huduma mbalimbali kwani kazi anayoifanya sio ya kwake bali ya Mungu aliye mtuma... unampata kwa no. 0674 411 705 - 0784 130 176

KUSIKILIZA WIMBO WA ENEZA, HUU HAPA