Tuesday, June 21, 2016

WIMBO WA MAUA WAZIDI KUNG'ARA... SASA UNAWEZA KUUPATA KAMA MWITO KWENYE SIMU...




Nyota Njema huonekana asubuhi, huu ni usemi wa kiswahili ambao watu wengi huutumia kama metrhali kama mimi pianinavyoutumia kuuzungumzia wimbo wa Maua wa kwake Beatrice Kitauli.
Wimbo huu ni wimbo ambao unatamba katika masikio ya watu kwa sasa kupitia vituo mbalimbali vya Radio hapa nchini na kwenye mitandao mingi ya Kijamii.
naweza kusema katika nyimbo bora ambazo zimekwisha kutoka katika mwaka huu, wimbo huu wa Maua unaweza kuchukua nafasi ya kwanza kwa uboza.
tunapozungumzia ubora tunamaanisha kuwa ni wimbo mzuri amboa unaongoza kupendwa na watu.
Wimbo huu sasa unaweza kuupata kama ring tone kwa kutuma ujumbe 2131032 kwenda 15050 Tigo Beat. kama ilivyoelekeza kweny picha hapo juu



Wimbo huu wa maua utapatikana pia katika Album ya MAUA ya kwake Beatrice Kitauli itayo kuwa mitaani hivi karibu. kinachosubiriwa ili album hii iingie mitaani ni video ambayo iko jikoni inaandaliwa chini ya kampuni ijulikanayo kama Kwetu Studio.
Beatrice anasisitiza kuwa video zitakuwa na kiwango cha hali ya juu na ambacho kitawafurahisha watazamaji wote.

Monday, June 13, 2016

ALBUM YA MAUA YAWA GUMZO HATA KABLA YA UJIO WAKE RASMI... WADAU WAFUNGUKA...



Katika hali isiyotarajiwa ujio wa Album ya  MAUA ya kwake Beatrice Kitauli, ambayo iko mbioni kuachiwa, imekuwa gumzo la jiji Kabla hata bado haijaachiwa na kuingia mitaani kwa wadau na wasikilizaji mbalimbai.
hali hii imetokana na wimbo unaobeba jina la Ulbum hiyo kuwafikia baadhi ya watu na kuona uzuri wa wimbo huo,

"... kusema kweli nilikuwa nikiona tu posti mbalimbali kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ikizungumzia ujio wa Album hiyo, kama kunapost ile ya SMAGAZINE, nilipoiona nikakuta kuna namba ya muimbaji Beatrice ikabidi niingie whatsap nikamuomba wimbo huo, yaani ni mzuri..." akisema kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la boniface.
 
lakini yvonne yeye anasema aliusikia kupitia redioni lakini hakumbuki ilikuwa ni kituo gani cha redio.
"... wimbo wa maua naufahamu nilishausikia kupitia redio lakini sikumbuki ilikuwa redio gani, kusema ule ukweli wimbo ni mzuri tunasubiri tuone video..."
alisema Yvonne.
Video ya Album ya MAUA ya kwake Beatrice Kitauli iko jikoni na yeye mwenyewe anawaambia mashabiki wake kuwa wategemee video yenye ubora wa hali ya juu.
"... hii itakuwa ni video tofauti na zile ambazo watu walizoea kuziona, video na matukio yatakuwa yanaendana na ujumbe uliomo kwenye nyimbo, nataka watu wajiandae tu kuona kitu kipya ambacho hawajawahi kukiona..." alimalizia beatrice.
Album ya maua ilitengenezwa katika Studio za Eck Production chini ya Produce Eck.

Thursday, June 9, 2016

ALBUM YA MAUA YA KWAKE BEATRICE KITAULI IMEKUWA GUMZO LA JIJI...



Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Tanzania Beatrice Kitauli ambaye anatamba sasa na Kibao kiitwacho MAUA, amesema sasa ni zamu yake kwani Album aliyoiandaa ni moto wa kuotea mbali.
akiongea kwa njia ya mtandao na mwandishi wa habari hizi, Beatrice amewatahadharisha wakongwe kwenye tasnia hii ya uimbaji wa nyimbo za injili kukaa chonjo kwani albumu ya MAUA itapiku album nyingi za wakongwe ambao wameonekana kulegalega katika uimbaji kwa wakati huu.
"... hii ni kazi ya Mungu tunayofanya lakini pia tunatakiwa kutumia vizuri vipaji tulivyopewa ili kuufikisha ujumbe kwa walengwa ukiwa katika hali nzuri, kusema kweli Album hii ya MAUA, sijisifii lakini nasema baadhi ya wakongwe wajihadhari kwani moto wa Album hii sio wa Kitoto..." alisema Beatrice.



Beatrice amesemakuwa Video ya Album hiyo ndio iko jikoni inatengenezwa chini ya kambuni iitwayo kwetu studio ambapo album hiyo inabeba jumla ya nyimbo Nane. ikiwa ni pamoja na 1. Maua, 2. Roho Yangu 3. Ole Wako 4. Acha Kuloga 5.Shamesha Vavae 6. Yupo Mungu 7. Niseme na Yesu na wa 8. Maua no.2
"... Kusema ukweli nawaomba watanzania watarajie kupata Video bora ambazo ni tofauti na zile zilizozoeleka, hizi zitakuwa nzuri na zinazoendana na Ujumbe wa nyimbo husika..." alimalizia Beatrice.
akasema pia kwa yeyote anayetaka kuupata wimbo wa Maua kupitia Whatsap anaweza kutumia namba hii kuupata. 0757 890 451

Friday, June 3, 2016

TB JOSHUA ATOA MSAADA KWA TANZANIA... AMKABIDHI MAMA MAGUFULI...

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli amemshukuru nabii TB Joshua wa Nigeria kwa msaada alioutoa kwa Tanzania baada ya kuongea nae na kumueleza maono yake ya kusaidia wazee na watu wenye ulemavu..
Mama Janeth amesema Namshukuru kwa msaada huu mkubwa aliotuwezesha katika kambi hii ya Wazee, nilipoongea nae nilimueleza maono yangu kwa ajili ya huduma hii ninayofanya ya kuhudumia Wazee, watu wenye ulemavu na wasiojiweza
Niliongea nae akasema ataniunga mkono na kama mnavyoona hapa leo yeye mwenyewe ametuma mwakilishi wake amenunua vyakula, namshukuru Nabii TB Joshua kwa kutoa, amekua akitoa misaada bila kujali itikadi za dini wala nchi… Mungu ambariki sana‘ Aliongea Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli