Monday, June 13, 2016

ALBUM YA MAUA YAWA GUMZO HATA KABLA YA UJIO WAKE RASMI... WADAU WAFUNGUKA...



Katika hali isiyotarajiwa ujio wa Album ya  MAUA ya kwake Beatrice Kitauli, ambayo iko mbioni kuachiwa, imekuwa gumzo la jiji Kabla hata bado haijaachiwa na kuingia mitaani kwa wadau na wasikilizaji mbalimbai.
hali hii imetokana na wimbo unaobeba jina la Ulbum hiyo kuwafikia baadhi ya watu na kuona uzuri wa wimbo huo,

"... kusema kweli nilikuwa nikiona tu posti mbalimbali kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ikizungumzia ujio wa Album hiyo, kama kunapost ile ya SMAGAZINE, nilipoiona nikakuta kuna namba ya muimbaji Beatrice ikabidi niingie whatsap nikamuomba wimbo huo, yaani ni mzuri..." akisema kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la boniface.
 
lakini yvonne yeye anasema aliusikia kupitia redioni lakini hakumbuki ilikuwa ni kituo gani cha redio.
"... wimbo wa maua naufahamu nilishausikia kupitia redio lakini sikumbuki ilikuwa redio gani, kusema ule ukweli wimbo ni mzuri tunasubiri tuone video..."
alisema Yvonne.
Video ya Album ya MAUA ya kwake Beatrice Kitauli iko jikoni na yeye mwenyewe anawaambia mashabiki wake kuwa wategemee video yenye ubora wa hali ya juu.
"... hii itakuwa ni video tofauti na zile ambazo watu walizoea kuziona, video na matukio yatakuwa yanaendana na ujumbe uliomo kwenye nyimbo, nataka watu wajiandae tu kuona kitu kipya ambacho hawajawahi kukiona..." alimalizia beatrice.
Album ya maua ilitengenezwa katika Studio za Eck Production chini ya Produce Eck.

No comments:

Post a Comment